Utafiti Mpya Waonesha Lowassa Kushinda Kwa Asilimia 74 Dhidi ya Magufuli - MULO ENTERTAINER

Latest

25 Sept 2015

Utafiti Mpya Waonesha Lowassa Kushinda Kwa Asilimia 74 Dhidi ya Magufuli

Siku mbili baada ya tahasisi ya TWAWEZA kutoa matokeo ya utafiti ukionesha kama ucaguzi ungefanyika kati ya august 19/2015 na septemba 7,2015 mgombea urais kupitia CCM angeshinda kwa aslimia 65 dhidi ya 25 za mgombea wa CHADEMA Edward Lowassa,leo vigogo wa chadema wamejitokeza mbele ya waandishi wa habari na kutoa matokeo ya utafiti wanaodai kufanywa na tahasisi za kimataifa unaonesha lowassa kushinda kwa aslimia 74.Mbali na matokeo hayo wamepinga utafiti wa TWAWEZA kuwa yalipikwa kuisaidia CCM.Hapa chini ndiyo waliyosemaMbatia: Taarifa ya Twaweza imeidhalilisha CCM na Twaweza yenyewe!
Mbatia: Twaweza imejidhalilisha kwa kubagua wagombea Urais wa vyama vingine mbali na CCM na CHADEMA!
Mbatia: Twaweza haifahamu hata idadi ya wagombea ubunge wala udiwani
Mbatia: utafiti wa Twaweza imetoa ripoti inayokinzana angalia ukurasa wa 7, huu ni utafiti wa uongo!
Mbatia: katika taarifa ya Twaweza haijaweza kuhakiki taarifa yake kitakwimu!
Mbatia: CCM imekubaliana na idadi ya watu walioshiriki utafiti wa Twaweza kwa kigezo cha idadi ya watu 1848!
Mbatia: CCM ilikataa kukubali maoni ya wananchi zaidi ya laki 3 kwenye rasimu ya Katiba ya Warioba, lakini leo wamekubali 1848
Mbatia: Taarifa ya Twaweza inalidhalilisha Taifa letu mbele ya dunia
Mbatia: kama taarifa ya Twaweza ingetolewa kabla ya Uchaguzi Mkuu ingevisaidia vyama.
Mbatia: simu za mkononi na chaja zilizogawiwa ilikuwa ni rushwa iliyotolewa na Twaweza kwa washiriki wa utafiti wao!
Mbatia: Twaweza imebatiza tafsiri ya UKAWA kuwa ni Walinzi wa Katiba ya Wananchi. Soma taarifa yao utaona ndivyo walivyoandika!
Mbatia: Twaweza wanajua CUF, NCCR-Mageuzi, na NLD hawajatoa Mgombea wao wa Urais isipokuwa CHADEMA, ila wameweka swali hilo
Mbatia: kwa kuwa Twaweza ni taasisi inayothamini midahalo, tunawaalika kwenye midahalo wa kuitetea taarifa ya utafiti wao
Mbatia: tunawaomba wapiga kura wote wasiitilie maanani taarifa hii ya Twaweza
Mbatia: hakuna taasisi yoyote iliyoleta mwaliko kwa Mgombea wetu Edward Lowassa kushiriki midahalo mpaka sasa!
Mbatia:Utafiti wa ndani wa UKAWA uliofanywa na watafiti huru kutoka nje ya nchi zinaonesha Edward Lowassa atapata asilimia 74 ya kura zote
Mbatia: utafiti wetu wa ndani uliofanywa na wataalamu kutoka nje ya nchi umeonesha Edward Lowassa atapata kura 74%
Prof. Baregu amezungumzia 'contamination of data' ya utafiti wa Twaweza
Prof.Baregu anazungumzia decay of data katika utafiti wa Twaweza
Prof.Baregu utafiti huu wa Twaweza sio wa kwanza. Mara ya kwanza utafiti wao wakati Edward Lowassa akiwa CCM ilionesha anaongoza
Prof.Baregu:Kama Dr.Slaa alizidiwa kura na Edward Lowassa miezi michache iliyopita, imekuwa leo Edward Lowassaazidiwe kura na Magufuli?
Prof.Baregu: Sampuli ya data za utafiti wa Twaweza imechafuliwa kwa makusudi ili kupotosha Watanzania.
Prof.Baregu: Mtafiti kutoka Oxford University niliyeongea naye aliona kuwa UKAWA inaweza kushinda ila sio kwa gap kubwa.