Africa’s 50 Richest (Forbes): Dewji ni Namba 21, Aongoza Tanzania - MULO ENTERTAINER

Latest

21 Nov 2015

Africa’s 50 Richest (Forbes): Dewji ni Namba 21, Aongoza Tanzania

Forbes wametoa orodha ya watu 50 matajiri zaidi barani Afrika.

Nafasi ya kwanza imeendelea kushikiliwa na bilionea wa Nigeria, Aliko Dangote mwenye utajiri wa dola bilioni 16.7.

Mwenyekiti Mtendaji wa METL, Mohammed Dewji amekamata nafasi ya 21 kwenye orodha hiyo akiwa na utajiri wa dola bilioni 1.1. Dewji anaendelea kuwa tajiri namba moja nchini Tanzania.

Rostam Aziz amekamata nafasi ya 25 kwa utajiri wa dola milioni 900 huku Said Salim Bakhresa akikamata nafasi ya 36 kwa kuwa na utajiri wa dola milioni 600.