Baada ya Alikiba kupost ujumbe katika Instagram akidai kuwepo na mambo yanayoendelea nyuma ya pazia kwenye muziki wake na wengi kutafsiri amelalamikia kukosa tuzo za Afrima, uongozi wa Diamond aliyeshinda tuzo tatu umezungumza.Akizungumza katika pindi cha XXL cha Clouds FM, mmoja kati ya mameneja wa Diamond, Babu Tale alisema walisikitishwa na ujumbe huo.“Mimi naona asiyekubali kushindwa sio mshindani,” alisema. “Hata sisi tumeshawahi kuingia kwenye tuzo ambazo na yeye aliongea maneno hayo alikuwepo na akashinda na hakuna mtu yeyote aliongea sijui mmenunua tuzo. Mimi nilijua mashabiki ndio wanaongea mpaka msanii anapost kitu kama kile nikahisi labda kuna mtu amehack akaunti yake. Kwahiyo nilivyoona vile nikamhukumu sio mshindani,” alisema Tale.
Hata hivyo Tale alisema baada ya kufuta kauli hiyo na kuzungumzia kauli hiyo aligundua huenda alishinikizwa na mashabiki wake.
“Lakini baadaye baada ya kuona ameongea vizuri, nikagundua sometimes mtu anaweza kupaniki kwa ajili ya mashabiki wanaoongea. Lakini mwisho wa siku tunatakiwa tukae meza moja ili tusukume muziki wetu wa Tanzania. Tukiangalia line up ya muziki wa Afrika sasa hivi tupo namba mbili, tunakwenda kwenye namba 1,” aliongeza.
Hata huvyo Alikiba aliifuta post hiyo na kudai kuwa hakuandika kwa sababu alikosa tuzo.
19 Nov 2015
New
Kauli ya Uongozi wa Diamond Baada ya Ali Kiba Kudai Diamond Ametumia Fedha Kupata Tuzo za Afrima
mulo
Newer Article
VIDEO! She Was Caught Doing It In The Parking Lot, Men Only, Ladies Keep Off.
Older Article
UKAWA Kumpokea Rais Magufuli Bungeni Kwa Staili Mpya
Tanasha na Diamond bado penzi lao la motoo!Jan 10, 2019
Daimond Akabidhiwa Shule SumbawangaDec 09, 2018
Labels:
Ally Kiba,
Diamond Plutnumz