Indonesia yasitisha utafutaji wa Air Asianiliyopotea hapo siku ya jana tarehe 28/12/2014 - MULO ENTERTAINER

Latest

29 Dec 2014

Indonesia yasitisha utafutaji wa Air Asianiliyopotea hapo siku ya jana tarehe 28/12/2014

A
Indonesia imesitisha utafutaji wa ndege ya AirAsia hadi kesho iliopotea na takriban abiria 160 waliokuwa wakielekea Singapore kutoka mji wa Surabaya nchini Indonesia.
Ndege za kijeshi kutoka indonesia na singapore zilikuwa zikiisaka ndege hiyo kusini magharibi mwa pwani ya Borneo ambapo ndege hiyo ilitoweka.
Takriban abiria 162 walikuwa wakiabiri ndege hiyo aina ya Airbus 320 wengi wao wakiwa raia wa Indonesia.
Ndugu na familia za waathiriwa wa AirAsia wakisubiri habari za kutweka kwa ndege hiyo
Rubani wa chombo hicho anadaiwa kutaka kubadilisha njia ili kuepuka kimbunga lakini hakuomba usaidizi wowote.
Baadhi ya meli katika eneo hilo zinaendelea kuitafuta ndege hiyo,licha ya hali mbaya ya hali ya anga
Familia na marafiki wa waathiriwa wamekongamana nchini Singapore na uwanje wa ndege wa surabaya wakingojea habari kuhusu ndege hiyo.