Lulu: Mapedeshee ndio wanawalipa wasanii wa kike siyo filamu - MULO ENTERTAINER

Latest

14 Jan 2015

Lulu: Mapedeshee ndio wanawalipa wasanii wa kike siyo filamu


ELIZABERTH Michael‘ Lulu’ amefunguka kuwa wasanii wa kike wa filamu wana biashara nyingine iliyojificha ndani ya ile ya filamu ambayo inawalipa zaidi.
Lulu amepasua kuwa wasanii hao wanawategemea mapedejee kuendesha maisha yao huku wengi wakiamini kwamba mabinti hao wa Bongo Movie wanalipwa vizuri kutokana na filamu wanazoigiza.

“Ukweli hauko hivyo, hali hii inatokana na wengi wetu kudumaa na hatuwazi kufanya mambo makubwa kwa kuigiza na wasanii wakubwa lakini hakuna anayeliona hili,” alifafanua.

“Hakuna anayefirikiria kuigiza na wasanii wa kimataifa kama Ritha Dominic ili sanaa imlipe na wengi wanawategemee mapedejee au biashara zisizo rasmi, kwani filamu inaonekana ipo juu lakini wahusika wake wanalipwa kwa staili nyingine kabisa,” alisema.