Michuano ya marudiano ya hatua ya 16 bora katika UCL yatarajiwa kuanza leo.
Timu mbili za kwanza zitakazoingia robo fainali ya mashindano ya Klabu Bingwa Barani Ulaya zinatarajiwa kubainishwa leo.
Mabingwa
watetezi Real Madrid walioibuka na ushindi wa magoli 2 – 0 ugenini
dhidi ya Schalke 04 katika mechi ya kwanza wanatarajia kujihakikishia
tiketi ya robo fainali. Schalke 04 nayo itakuwa na kibarua kigumu cha
kuipindua Real Madrid.
Kwingineko,
timu ya Porto itawakaribisha Basel nyumbani katika mechi
itakayobainisha mshindi atakayeingia robo fainali baada ya kutoka sare
ya 1 – 1 katika mechi ya kwanza.
Mechi hizo zinatarajiwa kuanza mwendo wa saa 21.45 usiku kwa nyakati za Uturuki.
