Wema Sepetu Aukana Wimbo Wa Diamond Platnumz - MULO ENTERTAINER

Latest

10 Mar 2015

Wema Sepetu Aukana Wimbo Wa Diamond Platnumz


Wakati hit single ya Diamond Platnumz, Ntampata Wapi inatoka mwaka jana, watu wengi waliamini kuwa wimbo huo amemwandikia ex wake, Wema Sepetu.

Tetesi hizo zilienea baada ya kubainika kuwa wawili hao wameachana tena. Hata hivyo Wema amedai kuwa si kweli.

“Leo nasema rasmi kuwa hii nyimbo hakuniandikia mimi,” Wema aliiambia Radio 5 ya jijini Arusha.

“Because nilikuwa naisikia hii nyimbo hata wakati tulipokuwa kwenye uhusiano alikuwa akiimba, akiind kwahiyo ilikuwa tu ni moja ya nyimbo zake kama anavyoandika nyimbo zote lakini nadhani tu timing ya kutoka ndio kidogo imekuwa na utata because kaitoa timing ambayo watu wote wakadhani kamuimbia Wema but in real sense noo,” aliongeza Wema.