Wasanii wa Kike Walio Katika Mapenzi na Wadogo Zao - MULO ENTERTAINER

Latest

24 Sept 2015

Wasanii wa Kike Walio Katika Mapenzi na Wadogo Zao

Aunt Ezekiel na Moze Iyobo

Mwigizaji wa filamu za bongo, Aunt Ezekiel, mwenye miaka 29, yupo kwenye mahaba mazito na Moze Iyobo, mwenye miaka 23, ambaye ni mnenguaji wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.

Kuzidiana huko kwa umri hakukuwafanya washindwe kuendeleza familia yao, kwa sasa wana mtoto mmoja. Aunt Ezekiel anasema: “Kitu muhimu katika uhusiano wetu ni mapenzi tunayopeana ambacho ndicho kitu tunachotaka katika uhusiano wetu na si suala la umri’’.



Shilole na Nuh Mziwanda

Mwingine ni Zuhena Mohammed ‘Shilole’, ambaye ni mwimbaji na mwigizaji wa filamu za Bongo, naye amedondokea katika mapenzi ya msanii mwenzake, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’.

Umri wa Shilole ni mkubwa kuliko wa Mziwanda, lakini ukubwa wa umri huo hauwazuii kujivunia mapenzi yao na kufanya mambo yao mengine kama kawaida, ingawa mara kwa mara mashabiki wao wamekuwa wakiwapigia kelele kuhusiana na umri wao, lakini majibu ya Shilole ni kwamba; “Sikushawishiwa na mtu kumpenda Nuh Mziwanda, bali moyo wangu ndiyo ulimpenda na hakika ananidatisha siwezi kutengana naye kwa kuwa ni mwanamume kama walivyo wanaume wengine,” hayo ni maneno ya Shilole.

Riyama Ally na Idd Mwalimu

Mwigizaji mwingine ni Riyama Ally, huyu humwambii chochote kwa msanii wa muziki wa kufokafoka (hip hop), Idd Mwalimu Mzee, aliyemchumbia hivi karibuni.

Ingawa Riyama anadaiwa kumzidi mpenzi wake huyo kwa miaka saba, lakini umri huo haumkatishi tamaa mwigizaji huyo, ambaye muda wote amekuwa akiweka wazi kwamba wamepanga kufunga pingu za maisha.