Huyu ndio mtoto aliyezaliwa na kuvunja rekodi ya kuwa na uzito mkubwa zaidi India.. - MULO ENTERTAINER

Latest

7 Oct 2015

Huyu ndio mtoto aliyezaliwa na kuvunja rekodi ya kuwa na uzito mkubwa zaidi India..

Kwenye Kitabu cha Kumbukumbu kubwa za Dunia, Guinness World Records kumbukumbu kubwa kuwekwa na mtoto aliyezaliwa na uzito mkubwa zaidi iliwekwa mwaka 1955 na mtoto ambaye alizaliwa akiwa na uzito wa Kilo 10 Italy.

Rekodi nyingine kubwa kwenye Kumbukumbu Marekani ni ya mtoto aliyezaliwa na uzito wa Kilo 6.8 mwaka 2014, lakini India nao wana Rekodi kubwa iliyowekwa kwa watoto wachanga wanaozaliwa.

Mama Goga Bai amejifungua mtoto wa kiume October 01 2015 na Rekodi ambayo mtoto wake ameiweka India ni ya kuzaliwa na uzito mkubwa zaidi ambao ni Kilo 5.9.

Daktari mmoja amesema huyo mtoto amevuja Rekodi ya kuzaliwa na uzito mkubwa zaidi kwa sababu wastani wa watoto  wanaozaliwa India ni kati ya Kilo 2.5 na kilo 3.5.

Mama huyo kajifungua salama kabisa na yeye pamoja na mtoto wake wako kwenye afya nzuri.