Kasi ya Magufuli ya Hapa Kazi tu Yasababisha Mrembo wa Bongo Movies Kuyakataa Mapenzi - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Jan 2016

Kasi ya Magufuli ya Hapa Kazi tu Yasababisha Mrembo wa Bongo Movies Kuyakataa Mapenzi


MSANII wa Bongo movies Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ amesema katika kipindi hiki cha kasi ya Rais John Magufuli, hana muda wa kuhangaika na mapenzi, badala yake yeye atachapa kazi tu.
Akizungumza na gazeti hili, msanii huyo alisema kumekuwa na wimbi kubwa la wezi wa mapenzi wanaotumia fedha, lakini kwake ni bora ajibidishe kivyake ili apate chake halali.
“Mimi naona kabisa hapa Bongo hakuna mapenzi, kuna usanii tu, kila mmoja anajidai yupo kwenye mapenzi kumbe utalii, ninachojua mimi hapa ni kazi tu mapenzi nchi za watu,” alisema.
Toa maoni yako