Msaniii AT Atoa ya Moyoni Kuhusu Mwanamuziki Ali Kiba..Awashangaa Watu Wanaosema Anaringa - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Jan 2016

Msaniii AT Atoa ya Moyoni Kuhusu Mwanamuziki Ali Kiba..Awashangaa Watu Wanaosema Anaringa

Mfalme wa miondoko ya mduara nchini AT, ambaye amewahi kutamba na nyimbo yake ya Bao la Kete na nyingine nyingi zilizo wakuna wadau wa muziki na kuamua kuongeza ushabiki mkubwa kwenye aina ya mziki huAT ameuamua kusema ukweli ambao alikuwa ameuhifadhi moyoni kwa muda mrefu juu ya mahusiano yake na msanii nyota kwa sasa nchini Tanzania, mwenye mashabiki wengi kutokana na tungo zake kuwagusa wengi ajulikanaye kama Alikiba hitmaker wa Nagharamia aliyofanya na Chrstian Bela.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram AT amemzungumzia Alikiba kama msanii mwenye kufanya jitihada katika kazi zake na mwenye kusaidia watu tofauti wa watu wanavyomdhania kuwa anaringa, jambo ambalo AT analipinga kwa asilimia mia moja kwa sababu kama angekuwa anaringa asingeweza kumsaidia yeye, kipindi hicho hana kitu.
MULO ENTERTAINER BLOG