Lulu Hakurudi Tanzania Jana… Ninacho Alichoandika Leo Kuhusu Kurudi Kwake Nyumbani na Tuzo - MULO ENTERTAINER

Latest

7 Mar 2016

Lulu Hakurudi Tanzania Jana… Ninacho Alichoandika Leo Kuhusu Kurudi Kwake Nyumbani na Tuzo

Tunajua ni Watanzania wawili walishinda tuzo mbili kwenye usiku wa tuzo za Africa Magic Viewer’s Choice Awards, wa kwanza ni Single Mtambalike ‘Richie’ na Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambapo Richie tayari alisharudi nyumbani Tanzania usiku wa March 6 2016 ila Lulu hakutokea Airport japo baadhi ya watu walimtarajia.

March 7 2016 Lulu amewajulisha Watanzania kwamba anarudi nyumbani siku ya March 8 2016 na atatua uwanja wa ndege Dar es salaam na akayaandika haya
 ‘Tukijaaliwa uzima…kesho saa 8:30 (saa nane na nusu Mchana) nitaingia uwanja wa ndege Dar Es Salaam na mzigo wenu😂au acha niseme Tuzo Yenu..!!💋💋💋Can’t wait to see y’all😍
(I’m hungry and I’m ready 4 change….TODAY👊)