Simba Ubingwa Ndio Basi Tena..Fifa Yatuma Ujumbe Huu Kwa Yanga - MULO ENTERTAINER

Latest

24 May 2017

Simba Ubingwa Ndio Basi Tena..Fifa Yatuma Ujumbe Huu Kwa Yanga



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani Fifa, Gianni Infantino ametuma salamu za pongezi kwa Klabu ya Dar es Salaam Young African kwa kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Kupitia ukurasa wa Twitter wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, Jamali Malinzi ameandika ujumbe huo ambao umetoka kwa Rais wa Fifa kwenda kwa Yanga SC akisema: “Rais wa FIFA Bw Gianni Infantino leo ametuma salam za pongezi kwa klabu ya Yanga kwa kushinda ubingwa wa Ligi Kuu.Ameitakia kheri Yanga.” – Malinzi.