Kim Kardashian: Sijathibitisha Chochote Kuhusu Mtoto Wangu - MULO ENTERTAINER

Latest

11 Sept 2017

Kim Kardashian: Sijathibitisha Chochote Kuhusu Mtoto Wangu


Kim Kardashian West Weekend hii amekiambia kipindi cha E!News America kuwa amesikia stori nyingi kuhusu ujio wa mtoto wake wa tatu ila hajathibitisha chochote.

Star huyu wa Keeping Up With the Kardashians ambaye ni Mke wa Rapa Kanye West tayari ana watoto wawili North West na Saint West na awali iliripotiwa kuwa anategemea kupata mtoto wa tatu ila mimba alibeba mwanadada mwingine ambaye alilipwa na familia hio.

Kim  anasema ”Nimesikia mambo mengi, stori zingine hata sijawahi kusikia, sijathibitisha chochote, tukiwa tayari tutaongea na kuwafahamisha”