Kura ya Kutokuwa na Imani na Zuma Kupigwa Bungeni Kesho - MULO ENTERTAINER

Latest

14 Feb 2018

Kura ya Kutokuwa na Imani na Zuma Kupigwa Bungeni Kesho

Kura ya Kutokuwa na Imani na Zuma Kupigwa Bungeni Kesho


Kura ya kutokuwa na imani na Rais Zuma kupigwa Bungeni kesho baada ya Rais huyo kutotekeleza wito wa kujiuzulu ndani ya saa 48

 Wabunge wa ANC wataitumia hoja ya kutokuwa na imani na Rais Zuma ambayo tayari imewasilishwa Bungeni na chama cha Upinzani cha Economic Freedom Fighters(EFF) kinachoongozwa na Mwanasiasa kijana mwenye makeke, Julius Malema

Tangu Rais Zuma aingie madarakani hoja 5 za kutokuwa na imani naye zimewasilishwa katika Bunge la Nchi hiyo huku 3 kati ya hizo zikikosa kura kutoka kwa Wabunge wengi na mbili zikikosa vigezo hivyo kutofanikiwa kupigiwa kura