- MULO ENTERTAINER

Latest

29 Dec 2014


Acha muvi iendelee! Ile projekti ya mastaa wakubwa Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’ sasa imenoga.
Mastaa wakubwa Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’wakila ujana.
Habari zinaeleza kwamba katika pati ya mwaka ya Zari wiki iliyopita iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Guvnor uliopo Kampala, Uganda mwanadada huyo hakuishia kwenye pati tu bali alitumia nafasi hiyo kumtambulisha Diamond aliyekuwa mgeni rasmi kuwa kwa sasa wao ni wapenzi.
‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari’ wakifanya yao.
Mbali na mahaba niue waliyooneshana mbele za watu, wawili hao walitumia chansi hiyo ‘kudendeka’ mbele ya kamera hivyo kudhihirisha kwamba mambo yao yapo juu ya mstari.