Polisi wafyatua risasi kuzuia vurugu jijini Dar - MULO ENTERTAINER

Latest

6 Jan 2015

Polisi wafyatua risasi kuzuia vurugu jijini Dar

Polisi Jijini Dar es Salaam wamelazimika kufyatua risasi hewani na kufyatua mabomu ya machozi kufuatia kuibuka kwa vurugu katika hoteli ya Land Mark ambapo shughuli ya uapishaji wa wenyeviti wa serikali Mitaa zinafanyika.
Vurugu hizo, zimeibuliwa na kambi ya upinzani ambayo imelalamikia kuwa Mwenyekiti mmoja wa Chama tawala CCM aliyeapishwa hakuwa ameshinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika mwaka jana.