Wakati Nyalandu Anakanusha Kuhusika na Mimba ya Aunty Ezekiel, Iyobo Nae Ana Haya..… - MULO ENTERTAINER

Latest

15 Feb 2015

Wakati Nyalandu Anakanusha Kuhusika na Mimba ya Aunty Ezekiel, Iyobo Nae Ana Haya..…

Baada ya hapo jana Waziri Lazaro Nyalandu kupitia Clouds FM kukanusha tuhuma  zilizokuwa zimezagaa kwenye magazeti  na mitandaoni za kuwa anachepuka na mwigizaji wa filamu hapa bongo, Aunty Ezekiel na kusisitiza kuwa yeye sio  muhusika wa ujauzito wa mwigizaji huyo, nikaamua kupitapita  kwenye kurasa za  mcheza shoo wa Diamond, Moses Iyobo ambae ndio 
anasemekana kuwa  yeye ndio amempa ujauziko mwigizaji  huyo.

Kwanza nilikutana na andiko la malalamiko kutoka kwa Iyobo, ambae alikuwa ameweka picha ya Aunty na kuandika haya;

Kama kumpenda nampenda sana lakini kinacho nipasua kichwa mie kuni save dalali kwenye cm yake yani sielewi ata kidogo

Lakini kilichonipa faraja ni picha hiyo hapo juu akiwa na Aunty kitandani na kuandika ule msemo kutoka Yamoto Band ambao unamaanisha mtu akipenda amependaaa.

‘Nzi kufa kwenye kidonda sio ufala ila..........’

Kwa picha na ujumbe huu ni wazi Iyobo ndio baba kijacho kutoka kwa Aunty Ezekiel.