Mwigulu Nchemba Achefukwa 'Sichafuki Kwa Uongo, na Uzushi Kama Huu ni wa Kupuuza' - MULO ENTERTAINER

Latest

12 Jun 2015

Mwigulu Nchemba Achefukwa 'Sichafuki Kwa Uongo, na Uzushi Kama Huu ni wa Kupuuza'

Ndugu zangu, uongo wa aina hii tena unapotolewa hadharani ni aibu kwa Taifa. Kwanza mimi nimeanzia mizunguko Pemba na Unguja na nimekwenda kwa ndege na niliondoka kwa ndege Dodoma.

Wewe unasema natumia gari la Serilikali, yaani uvushe gari la serikali mpaka Pemba na Unguja?

Pili vijana wote uliowataja na kuwaita masalia wapo Dar na Dodoma halafu mpaka sasa hakuna eneo nimetoa hela yoyote ile kwenye hili suala.

Uongo wa aina hii ni ukosefu wa maadili, ukosefu wa uungwana na ukosefu wa hofu ya Mungu.

Mbali na hapo hakuna Mkoa uliopo bara nilioanza kutafuta wadhamini. Hivyo basi, tuhuma hizi ni Uongo, Uzushi na unatakiwa kupuuzwa.