Diamond Asema Yuko Tayari Kufanya Collabo na Msanii Yeyote Tanzania Lakini Mwenye Vigezo Hivi - MULO ENTERTAINER

Latest

9 Jul 2015

Diamond Asema Yuko Tayari Kufanya Collabo na Msanii Yeyote Tanzania Lakini Mwenye Vigezo Hivi

Diamond Platnumz amesema kuwa yuko tayari kufanya collabo na msanii yeyote wa Tanzania, ambaye atakuwa anakidhi vigezo vyake.

Muimbaji huyo wa ‘Nana’ ameyasema hayo baada ya kuulizwa kwanini hafanyi collabo nyingi na wasanii wa Tanzania.


  • “Mimi sina tatizo as long as nijue hiyo kazi unayotaka kufanya na mimi itafika wapi,” alisema Diamond kupitia Clouds E.



  • “umejipanga vipi project yako na umeiandaa vipi, kwasababu sitaki nifanye tu nyimbo mwisho wa siku halafu iishie tu ndani unaiskiliza wakati natumia muda kukaa kuandika kupoteza muda studio.“