ROSE MHANDO Amkimbia Meneja Wake - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Jul 2015

ROSE MHANDO Amkimbia Meneja Wake

NYOTA wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando anadaiwa kumkimbia meneja wake, Alex Msama licha ya kuwepo kwa makubaliano kati yao yaliyohusu kulipiwa deni la kiasi cha shilingi milioni sita alizokuwa akidaiwa msanii huyo mwenye jina kubwa.

Alex Msama ambaye ni meneja wa Rose muhando.

“Meneja wake alikubali kumlipia pesa zote (6,500,000) ambazo Rose alikuwa anadaiwa baada ya kushindwa kuhudhuria tamasha moja huko mikoani, alitakiwa baada ya siku chache aingie studio kufanya kazi, lakini ametoweka na haifahamiki yupo wapi,” kilisema chanzo chetu.

Msama alipotafutwa alikiri kutokea kwa tukio hilo, akisema haeleweki Rose ana matatizo gani kwani walikubaliana baada ya siku chache aingie studio na kurekodi, lakini mpaka hivi sasa haijulikani alipo na hata simu yake ya mkononi haipatikani.
GPL

Gazeti hili lilimtafuta Rose bila mafanikio kwani simu yake haikuwa hewani.