Shamsa Ford:Naomba USINITESE, USINIUMIZE NA USINILIZE, Kama Sina Thamani Yoyote Kwako Naomba Ukae Mbali na Mimi .... - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Jul 2015

Shamsa Ford:Naomba USINITESE, USINIUMIZE NA USINILIZE, Kama Sina Thamani Yoyote Kwako Naomba Ukae Mbali na Mimi ....

Nina upendo kwa kila mtu bila ubaguzi, naishi maisha yangu halisi wala siigizi, nina huruma kwa kila mtu, sipendi ugomvi na mtu.

Nakuomba na wewe binadamu kabla hujafikilia kunibania riziki yangu kumbuka nina mtoto ambae anahitaji hiyo riziki.

Wewe binadamu kabla hujanifanyia ubaya wowote kumbuka nina mtoto ambaye kitamuumiza zaidi ya mimi coz furaha yake ni kumuona mama yake.

Wewe binadamu kabla ya kutaka kuniumiza na kutaka kunipa stress za kijinga naomba umfikilie mwanangu ambaye ananitegemea mimi.

Ukinipa stress nitashindwa kufanya kazi na mwanangu atakosa haki zake za msingi.

Naomba wewe binadamu USINITESE,USINIUMIZE,USINILIZE, kama sina thamani yoyote kwako naomba ukae mbali na mimi kuliko kuwa mnafiki kwangu au kwa ajili ya masilahi yako binafsi....

Shamsa Ford on instagram