DR Slaa Kuibukia CCM, Apangwa Kujitokeza Kwenye Mkutano wa CCM Jagwani..... - MULO ENTERTAINER

Latest

22 Aug 2015

DR Slaa Kuibukia CCM, Apangwa Kujitokeza Kwenye Mkutano wa CCM Jagwani.....



USHAWISHI mkubwa umefanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhakikisha kuwa, katibu mkuu aliye mapumzikoni wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wallboard Slaa anashiriki kwenye kampeni ya chama hicho tawala, Uwazi Mizengwe limeambiwa. Chanzo kutoka ndani ya CCM kilisema hivi karibuni kuwa, mazungumzo yamefanikiwa kwa kiwango kikubwa na kwamba upo uwezekano wa asilimia 90 kwa Dk. Slaa kupanda jukwaani siku ya ufunguzi wa kampeni za CCM uliopangwa kufanyika kwenye Viwanja vya Jangwani, Dar keshokutwa Jumapili. “Ili kukabili nguvu ya upinzani tulipanga kuwa Dokta atoke mafichoni ashiriki nasi kwenye uzinduzi, tuna imani hilo litafanikiwa na utakuwa ni mtaji mkubwa kwa chama chetu kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu,” kilisema chanzo chetu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI