Davido Atangaza Ujio wa Collabo yake na Joh Makini - MULO ENTERTAINER

Latest

19 Sept 2015

Davido Atangaza Ujio wa Collabo yake na Joh Makini

Hakuna surprise nzuri kama ile ambayo hukuwahi kuona hata dalili, na kwenye muziki hasa kwa msanii wa Bongo hakuna kitu kizuri kama msanii mkubwa wa nje kuanza kutease ujio wa kazi yenu hata kabla yako.

Ndicho kilichotokea usiku wa Sept 18 pale staa wa Nigeria, Davido alipotweet kuwa kuna collabo yake na Joh Makini inakuja.

Bado haijajulikana kama ni wimbo wa Davido kamshirikisha Joh Makini au Joh kamshirikisha Davido au ni wa wote.

Hii ni hatua nyingine kubwa ya safari ya Joh Makini kwenda kimataifa, baada ya kufanya collabo na AKA na kuwa kwenye matayarisho ya kufanya collabo nyingine na rapper KO wa Afrika Kusini, mashabiki wa rapper huyo wa Weusi watarajie collabo hiyo ya Davido na Mwamba wa Kaskazini.