Magufuli Utaua Mawaziri Waliopita Kwa Njaa, Hawana Cha Kufanya - MULO ENTERTAINER

Latest

1 Jan 2016

Magufuli Utaua Mawaziri Waliopita Kwa Njaa, Hawana Cha Kufanya

Mh. Magufuli kwanza nikupongeze kwa kazi nzuri uliyoifanya mpaka sasa, japo sijutii kura yangu niliyompa mamvi na wala sitakaa nijutie, tulikuwa tunataka mabadiliko na sasa ninayo furaha ya dhati kabisa kuyaona haya mabadiliko kupitia kwako

Pili Mh. Nilichofurahi zaidi ni kupunguza gharama kubwa za kuhudumia wizara na mawaziri wake 60 wa awamu iliyopita hakika wewe ni mzalendo, na samia pia najua aliupata uzalendo zaidi katika kipindi za kampeni kijiji kwa kijiji nilimshuhudia akimwaga chozi kwa shida za wananchi alizokumbana nazo huko vijijini hakuamini na alituahidi na wasanii wakiwepo(mashahidi) mtaipitia mikataba yote ya madini

Mh. Magu chukua hii kama New year special, ulivyowatimua wastaafu mawaziri kwenye nyumba za serikali wengine hawana pa kukaaa, hakya Mungu tena ninaapa, hawakuona umuhimu wa kujenga kwa maana walijua nyumba za serikali ni zao

so sad , kuna mmoja anakaa kwa shemeji yake, (kaka wa mke wake) amechoka vibaya, sasa mbaya zaidi kaja na kuku wake kila siku wanatifua bustani za majirani maana humo ndani hamna banda wanafugia nje inaleta usumbufu mno, na hataki kuondoka mpaka ahakikishe kwamba hata ukuu wa wilaya amekosa ndio atarudi mwanzaaaa

Ninachokuomba Mh. harakisha hizo teuzi usifanye kwa nukta nukta utaua watu na njaa, hawana pa kuishi, hawana kazi, ubunge wamekosa, january hii watoto adaa mheshimiwa ujue hawasomi shule za kata, soon watakosa chakula na mimi ninasema ikifika february kuku wake wakiendea kutifua bustani yangu nakula mmoja baada ya mmoja