Ukawa, Tayari Jiji la Dar Lipo Chini yetu Pambanane na Changamoto Zilizopo - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Jan 2016

Ukawa, Tayari Jiji la Dar Lipo Chini yetu Pambanane na Changamoto Zilizopo

Jiji la Dar es Salaam kuwa sasa lipo chini ya Ukawa ni muda sasa wa Ukawa kupambana na changamoto nyingi za Jiji hilo baada ya kupata mameya na manaibu meya Kinondoni na Ilala.
Tatizo kubwa la foleni kwenye jiji la Dar esa Salaam pamoja uchafu mwingi unaozalishwa ni muda wa Ukawa kutatua ili tatizo.
Pia changamoto ingine ni mfumo wa leseni za biashara maeneo ya Ilala na Kinondoni imekuwa kero kubwa kwa wafanyabiashara ni wakati sasa wa Ukawa kupambana na ili suala la leseni.
Changamoto ingine hii mifumo ya ulipaji uhuru wa masoko kama Tandale, Kariakoo, Buguruni na maeneo mengine ni wakati sasa wa Ukawa kulisimamia ili suala hili wananchi wafanye biashara zao bila usumbufu.
Suala la parking kwenye Jiji la Dar es Salaam ni kero kubwa ni wakati sasa wa Ukawa kulitatua wananchi pamoja na malipo ya parking. 
Usumbufu mkubwa wa ukamataji ovyo wa boda boda na bajaji hii ni miradi ya watu ni wakati sasa wa Ukawa kulisimamia hili.
Toa Maoni yako