Ni kweli Clouds Media ndo Referee wa Game ya Muziki hapa Tanzania? DJ Choka Afunguka - MULO ENTERTAINER

Latest

10 Feb 2016

Ni kweli Clouds Media ndo Referee wa Game ya Muziki hapa Tanzania? DJ Choka Afunguka

Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu dhidi ya Clouds Media..Wasanii na watu mbalimbali wamekuwa wakiwatuhumu hawa jamaa kwa unyonyaji,ukandamizaji,uonezi n.k

Hata tumewahi kumsikia P funk kwa kauli yake akisema Clouds fm ndo chanzo cha marehemu Albert Mangwea kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya..
Ukiachia malalamiko mengi ya baadhi ya watu..Pia tumeshashuhudia Ugomvi mkubwa(ambao hata baadhi ya watu walidiriki kusema ulibeba sura ya kitaifa) kati ya clouds Fm na Mh. Sugu na hata ule wa Jay dee na Clouds Fm..Tuhuma zikiwa ni zilezile za uonezi,dhuluma,Ukandamizaji nk

Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Mkasi..Dj Choka akiwa ndo mgeni mwalikwa...Ikumbukwe wakati wa ugomvi wa Clouds na Jay Dee..Dj Choka alikuwa anamsapoti Lady Jay dee...Moja ya swali aliloulizwa kwenye kipindi ni kuwa ule ugomvi ulimuathiri vipi...Dj Choka alisema moja ya athari aliyoipata ni Nyimbo zake alizokuwa akitengeneza(Megamix) kutopigwa katika radio hiyo..

KITU KILICHONISHANGAZA
Dj choka alienda mbali zaidi na kusema kitendo cha kazi zake kutopigwa katika radio hiyo kilimfanya ASITISHE KUTENGENEZA KAZI mpaka hapo atakapoweka mambo sawa..

Kauli hii ya dj choka na baadhi ya malalamiko ya muda mrefu ya baadhi ya watu na wasanii yakanipa shauku ya kutaka kujua kama kweli Clouds media ndo referee wa hii industry bongo..

Na mengine ninayojiuliza ni pamoja na
1-Tz kuna zaidi ya vituo 50 vya radio..kwann clouds?
2-Clouds media wana nguvu kiasi gani inayowafanya wasanii wengi waamini kuwa clouds ndo wameibeba future yao?
3-Hiyo nguvu hawa jamaa wanaitoa wapi?