Nchi 10 Zinazolipa Vizuri Mishahara Duniani... - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Jul 2016

Nchi 10 Zinazolipa Vizuri Mishahara Duniani...

Je, ulishawai kujiuliza nchi ambazo wafanyakazi wanalipwa mishahara ya juu? Hebu tuangalie nchi kumi ambazo wafanyakazi wanapata malipo makubwa ya kazi zao wanazofanya


#10 Ufaransa
Ufaransa ni nchi ya 7 yenye uchumi mkubwa zaidi duniani, Wafanyao kazi Ufaransa wanafanya kazi kwa mda mchache ni kama masaa 35 kwa wiki. Kwa wastani  kipato cha mfanyakazi wa Ufaransa ni $28,799 kwa mwaka baada ya kulipa kodi zote.


#9 Sweden
Kutokana na data za Bank kuu ya dunia,hii nchi nzuri ya kiscandinavia ni ya sita kwa uchumi wa ndani duniani. Sweden ni wazalishaji wakubwa wa mbao. Kwa wastani kipato chao ni $29,185 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi


#8 Canada
Canada majirani wa Marekani,ni nchi ya tatu yenye uhifadhi mkubwa wa mafuta duniani ikipitwa na
Venezuela na Saudi Arabia. Nchi hii pia ina utajiri mkubwa wa zinc, uranium, dhahabu na aluminium.
Kwa wastani kipato chao ni $29,356 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi


#7 Austria
Austria ni nchi ambayo ipo katikati ya Ulaya, Imeendelea sana kiviwanda na sekta ya utalii
inachangia asilimia 9 ya pato la ndani la taifa. Kwa wastani kipato chao ni $31,173 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi


#6 Germany
Germany ni nchi ya kwanza yenye uchumi mkubwa zaidi ulaya. Kwa wastani kipato chao ni $31,252 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi



#5 Australia
Australia ni moja kati ya nchi zenye uchumi imara zaidi duniani,ni wasafirishaji wakubwa wa madini na wanaagiza bidhaa chache sana kutoka nje.Katika swala la wastani wa utajiri, Australia ilishika nafasi ya pili duniani baada ya Switzerland mwaka 2013. Kwa wastani kipato chao ni $31,588 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi


#4 Switzerland
Uswisi inashika nafasi za juu katika utendaji bora wa serikali yao, ikiwa ni pamoja na uwazi wa serikali yao, uhuru wa raia, ubora wa maisha, ushindani wa kiuchumi na maendeleo ya binadamu. Kwa wastani kipato chao ni $33,491 kwa mwaka na wanafanya kazi masaa 35 tu kwa wiki.


#3 Norway
Norway ina utajiri mkubwa  wa maliasili ikiwa pamoja na mafuta,umeme wa maji,uvuvi na madini.Kwa wastani kipato chao ni $33,492 kwa mwaka


#2 Luxembourg
Luxembourg ni wasambazaji wakubwa wa chuma ulaya. Kwa wastani kipato chao ni $38,951 kwa mwaka


#1 USA
Pato la ndani kwa mwaka ni $55,000 na makato ya taxi ni asilimia 23.Wafanyakazi wa Marekani wanafanya kazi masaa 44 kwa wiki.