Alichoongea H Baba kuhusu nyumba walizopost Alikiba na Diamond - MULO ENTERTAINER

Latest

26 Oct 2016

Alichoongea H Baba kuhusu nyumba walizopost Alikiba na Diamond

Jana October 25, 2016 kwenye mtandao wa Instagram kulikuwa na majibizano ya mashabiki wa mastaa wakubwa wa muziki wa Bongo Flava Tanzania nawazungumzia Diamond Platinumz na Alikiba hukua akiwepo mtu wa kati H Baba ambaye pia aliwahi kutofautiana na Diamond Platinumz siku za nyuma na sababu ikitajwa na kuwa waliibiana nyimbo studio.
Kupitia account ya Instagram ya Diamond Platinumz jana alipost picha akiwa kwenye nyumba yake anayodai kuwa ameinunua nchini Afrika Kusini na kwa mujibu wake alikua amefika hapo kwa mara ya kwanza tangu alipoinunua nyumba hiyo. Na baada ya muda mfupi pia kuna picha zilianza kusambaa zikimuonesha Star single ya Aje, Alikiba akiwa kwenye nyumba iliyodaiwa ni yake pia. 
Sasa msanii H Baba naye aliamua kupost maneno kwamba kama kweli nyumba hizo ni zao basi wangepost documents za kuonesha wakizinunua na sio picha tu.
“Siku zote mimi ninachojua mtu anayependa kuwatangazia watu ni mstaarabu sana na kitu cha kwanza mtu anaponunua nyumba lazima apewe mkataba then angepiga picha akiwa anasaini sio wanatupostia picha tu. Anapost picha kwasababu Alikiba amepost nyumba na yeye ndio apost? Unatakiwa kumpongeza tu muziki ni ushindani sio kujibizana kwa picha”:- H Baba
Kupata full story, Play hapa chini.