Nahitaji kumuua Young D wa zamani- Young D - MULO ENTERTAINER

Latest

11 Oct 2016

Nahitaji kumuua Young D wa zamani- Young D

Rapa Young Dar es Salaam alimaarufu kama Young D amesema kwamba huu ni wakati wake kumuua yule Young D wa zamani na kurudi kivingine akiwa na mtazamo mpya vichwani mwa watu na mashabiki zake.


Young D alisema hayo kupitia kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz kinachorushwa na EATV Ting'a namba moja kwa vijana, Young D anasema baada ya kutangaza rasmi kuacha ngada mfumo wake wote wa maisha ameubadili ili kuweza kumfuta yule Young D ambaye watu walimfahamu na kumjenga Young D mpya.

"Mfumo wangu wote wa maisha ulikuwa haupo sawa hivyo Chochote nachofanya saizi kama hakinipeleki kwenye siku yangu ya mafanikio basi hakina nafasi kwenye maisha yangu, ni vitu ambavyo naamua mimi mwenyewe kama mtoto wa kiume kuna muda naamua kuwa hiki ni kwa ajili ya maisha yangu, mimi hapa nina Mama yangu na familia inaniangalia hivyo maamuzi niliyoamua ni kuikana nafasi yangu, yaani nataka nimuuwe yule Young D wa zamani pia nimlete huyu Young D mpya ambaye huyu mpya atawafanay watu wamsahau yule wa zamani kama aliwahi kuwepo" alisema Young D