ALI Kiba na Ommy Dimpoz Katika Kashfa ya Kutokumlipa Aliyewatungia Nyimbo ya Kajiandae - MULO ENTERTAINER

Latest

20 Dec 2016

ALI Kiba na Ommy Dimpoz Katika Kashfa ya Kutokumlipa Aliyewatungia Nyimbo ya Kajiandae


Zimetufikia za kunyapia nyapia kutoka shirika la wambea SHILAWADU kuihusu hitsong ya wakali wawili wa muziki hapa Bongo Ommy Dimpoz naAlikiba na ngoma yao ya Kajiandae.

Inasemekana kuna mtu  afahamikae kama Devi Zinda ambaye anadai kuwa kauandika wimbo huo na hapo awali alilipwa shilingi za kitanzania Laki 5 (500,000) na Ommy Dimpoz kama malipo ya wimbo huo na kuahidiwa kumaliziwa kitita kingine cha shilingi laki 5 ili kutimia million 1 kama ilivyokuwa makubaliano ya malipo ya uandishi wa wimbo huu