Jeshi la Polisi Latoa Ufafanuzi Juu ya Kuokotwa kwa Mwili wa Mtu Ufukwenu - MULO ENTERTAINER

Latest

14 Feb 2018

Jeshi la Polisi Latoa Ufafanuzi Juu ya Kuokotwa kwa Mwili wa Mtu Ufukwenu

Jeshi la Polisi Latoa Ufafanuzi Juu ya Kuokotwa kwa Mwili wa Mtu Ufukwenu


Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondon ACP Murilo Jumanne Murilo amezungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa jeshi hilo limeokota mwili wa mwanaume anayekadiriwa kuwa na miaka 35, katika eneo la ufukwe wa Coco Beach akiwa amefariki.

Kamanda Murilo ameeleza walipata taarifa ya kuonekana kwa mtu huyo kutoka kwa msamaria mwema na walipokwenda eneo la tukio waliukuta mwili wa mtu huyo ukiwa na majeraha na akiwa tayari ameshakufa.

Ameeleza kuwa Jeshi  la Polisi tayari limeanza mara moja kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo cha mtu huyo.