'Mimi Bado ni Chuma Cha Reli Nina Lipa , Nikiamua Kuolewa Naweza Tena Bila Shida' Monalisa - MULO ENTERTAINER

Latest

14 Jan 2015

'Mimi Bado ni Chuma Cha Reli Nina Lipa , Nikiamua Kuolewa Naweza Tena Bila Shida' Monalisa

Mwigizaji mkongwe wa filamu hapa  Bongo, Yvonne Cherly ‘Monalisa’ (33) amesema kuwa yeye siyo gubegube kwani alishawahi kukaa ndani ya ndoa lakini sasa ameamua kutulia.
Yvonne Cherly ‘Monalisa’
Akipiga stori mbili-tatu na  Gazeti la Uwazi, Monalisa alisema kuwa hata kama akiamua kurudi upya kwenye ndoa anaweza na kutilia msisitizo kuwa mwanaume atayemuoa lazima atambue kuwa anayemuoa ni Yvonne Cherly na si Monalisa kwani jina hilo litakalokuwepo kwenye cheti cha ndoa.

“Mimi si gubegube, nikiamua kurudi na kufunga ndoa naweza tena nitaolewa kama Yvonne Cherly kwani ndilo jina langu halisi. Ninachokiwaza kwa sasa si kukaa ndani ya ndoa bali namna kazi zangu zitakavyoweza kuonekana zaidi,” alisema Monalisa.