Napata shida sana kujua dhamira ya Mh Lowassa kwa Taifa la Tanzania na katika Siasa za Tanzania - MULO ENTERTAINER

Latest

5 Aug 2015

Napata shida sana kujua dhamira ya Mh Lowassa kwa Taifa la Tanzania na katika Siasa za Tanzania

1: Aliangaika sana kwa hali na mali kwa kutumia Pesa nyingi sana ndani ya CCM ili siku moja aweze kuwa Rais.

2: Kama angefanikiwa ndani ya CCM angetawala nchi kwa kufuata Sera za CCM na kudumisha Muungano wa Tanzania.

3: Leo hii amewakana CCM kwa kusema 'CCM si baba yangu wala mama yangu' kwa kutumia Pesa nyingi saana na kuhamia CHADEMA. Kama leo hii CCM imekanwa basi na wewe ukiwa kama mwanachama wa CHADEMA/UKAWA au Mwananchi wa kawaida wa Tanzania basi na wewe jiandae kukanwa wakati wowote.

4: Ametumia Pesa nyingi sana kuwashawishi CHADEMA na wengine (kuwanunua) ili awe mgombea pekee wa Urais kupitia UKAWA. Hii inaonesha wazi wazi ni jinsi gani Mh Lowassa hasivyopenda Demokrasia ya kweli na kupenda Uditekta kwa chochote atakacho.

5: Hivi Sasa amehamia CHADEMA kwa matumaini kwamba atashinda Urais na kama akifanikiwa basi atakuja kutawala nchi kwa kutumia sera za CHADEMA/UKAWA na kuvunja Muungano wa Tanzania na kuweka Serikali tatu.

Nikiwa kama Mwananchi nisiye na Chama chochote cha Siasa hapa Tanzania, napata shida saana kujua dhamira ya Mh Lowassa katika Siasa za Tanzania, napata shida sana kujua dhamira yake ndani ya Tanzania kitu ambacho kinanifanya KAMWE siwezi kumuamini chochote asemacho kuhusu swala lolote ndani ya Tanzania, kitu ambacho kinanifanya kutoamini chochote wasemacho CHADEMA/UKAWA maana kama wanaweza kununuliwa kwa mabilioni machache basi ata rasilimali za nchi na Serikali yao siku wakishika madaraka inaweza kununuliwa na Mataifa ya nje kwa pesa ndogo sana.

Kwa kutumia uzoefu wangu wa kutambua watu, Vitu vyote afanyavyo na matendo yake nayaona ni kama mchezo wa kuigiza and its too Good to be true haswa haswa sura yake ukiiangalia kwa makini sana you will see theres something fishy going on.

Kama kweli anauchukia Umasikini na anauchukia umasikini wa Watanzania basi katika mabilioni aliyoyapoteza kwenye Kampeni za kutaka kuwa Rais kupitia tiketi ya CCM na mpaka sasa CHADEMA/UKAWA basi kwanini asingetoa kiasi kidogo kwa Wananchi wa Tanzania na kuwasaidia??!

Je Mh Lowassa una dhamira gani ndani ya Tanzania, Je ni nani anayekutumia kuusaka Urais kwa namna hiyo?? Kwa malengo gani haswa??!

Watanzania, CHADEMA/UKAWA na vyama vyote vingine vya Siasa nchini muogopeni Mh Lowassa zaidi ya Ukoma, CCM wameona basi nanyi kuweni makini sana.

Asanteni.