NORA: Niliingia Vitani na Johari, Kisa Mapenzi! - MULO ENTERTAINER

Latest

17 Oct 2016

NORA: Niliingia Vitani na Johari, Kisa Mapenzi!

KUTOKA moyoni! Bila kumtaja mwanaume husika, mwigizaji wa kitambo Bongo, Nuru Nassoro ‘Nora’amekiri kuwahi kuingia vitani na staa mwenzake, Blandina Chagula ‘Johari’ kisa kikiwa ni kugombeapenzi la mwanaume mmoja maarufu jijini Dar (jina ni siri yake).


Katika mahojiano maalum na gazeti hili, Nora alifunguka kuwa hali hiyo ilitokana na maisha ya usichana yaliyochangiwa na umaarufu na umri.

“Huyo mwanaume alikuja kwa lengo la kunitaka lakini nikawa nahisi kama Johari na baadhi ya rafiki zake walitaka kuninyang’anya, nikaamua kumvaa Johari,” alisema Nora ambaye kwa muda mrefu alikuwa haivi na Johari.