Uchaguzi Kenya: Uhusiano wa KENYA na Tanzania Kuwa Shakani iwapo.......!!! - MULO ENTERTAINER

Latest

7 Aug 2017

Uchaguzi Kenya: Uhusiano wa KENYA na Tanzania Kuwa Shakani iwapo.......!!!

Kesho ni siku ya Uchaguzi Mkuu nchini Kenya na viashiria vinaonesha kama ilivyokawaida kwa Tawala za Kiafriak,Rais aliyeko Madarakani kwa sasa Uhuru Jomo Kenyata huenda akashinda kwa kishindo dhidi ya mpinzani wake Raila Omolo Odinga.

Kama ndivo itakavokuwa basi huenda matokeo hayo ya kaanzisha mnyukano mwingine mpya kabisa ndani ya Afrika Masharaiki. Nitaeleza. Kampeni za uchaguzi zimehitimishwa juzi Ijumaa kule jijini Nairobi huku Edward Ngoyayi Lowassa akimpigia kampeni za nguvu Uhuru Jomo Kenyata mgombea wa tiketi ya JUBILEE. Edward Ngoyayi Lowassa ni PM mstaafu wa Tanzania na ndiye aliyekuwa mgombea wa Urais Tanzania mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA under UKAWA na kuwa mshindi wa 2 kwa JPM akizoa takribani kura miilioni 6 na ushei.

Raila Omolo Odinga mgombea Urais kwa tiketi ya NASA ni rafiki kipenzi wa Rais wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli. Hapa ndipo kwenye kiini cha sintofahamu baada ya matokeo ya Uchaguzi nchini Kenya hapo 8/8/2017. Ikumbukwe kwamba Raila Omolo Odinga anachuana vikali na Uhuru Kenyata wa JUBILEE. Raila ni PM mstaafu nchini Kenya wakti wa awamu ya Mwai Kibaki. Je, nini kitatokea katika uhusuano wa Kenya na Tanzania kama Uhuru Kenyata atashinda ambaye anasaidiwa wenya kampeni na Edward Lowassa mpinzani wa Magufuli? Yamkini mambo yatakuwa supa iwapo Raila Jaramogi Oginga Odinga atashinda ambaye ni rafiki kipenzi wa John Pombe Magufuli. Tusubiri hatima ya mchuano huu kwani bado masaa machache tu kuingia siku ya 8/8 ifikapo usiku wa manane. Mungu ibariki Kenya, Mungu ibariki Tanzania na Mungu ibariki Afrika na watu wake.Amina.