Steve Nyerere: Kero za Kinondoni zimenifanya nigombee Ubunge - MULO ENTERTAINER

Latest

23 Jun 2015

Steve Nyerere: Kero za Kinondoni zimenifanya nigombee Ubunge

Msanii wa filamu za Kibongo,Steve Mengere’Nyerere’ hivi karibuni alitangaza nia ya kugombea ubunge kupitia jimbo la Kinondoni.

Aidha Steve alisema kuwa Kinondoni ndipo alipozaliwa na kukulia na anajua changamoto zinazowakabili wakazi wa jimbo hilo ambazo ni wakati wa mvua wananchi hukubwa na mafuriko lakini hakuna kiongozi aliyeweza kutatua tatizo hilo.

Pia aliongeza kuwa mikopo midogo midogo kwa kina mama na ajira kwa vijana,ongezeko la ada mashuleni ,kero ya uchafu ,tiba kwa akina mama wajamzito ambapo kwa sasa hivi mama mjamazito mzazi anapoenda kujifungua anaambiwa aende na pamba, mkasi n.k, vitanda kuwa vichache kwenye wodi zote. Gari la wagonjwa ni mmoja tu.