Lowassa: Wabunge na Mameya Wasiowajibika Tutawafukuza CHADEMA - MULO ENTERTAINER

Latest

19 Jan 2016

Lowassa: Wabunge na Mameya Wasiowajibika Tutawafukuza CHADEMA



Lowassa ameyasema hayo wakati wa kikao maalum na Mameya na Manaibu wao kutoka Manispaa ya Ilala na Kinondoni waliokwenda kumuona na kumpongeza kwa kuwawezesha kushinda katika Manispaa za Ilala na Kinondoni.

Alisema wameishakubaliana kama wabunge na Madiwani watashindwa kuonyesha uwezo wa kufanya kazi za wananchi katika mwaka wa kwanza na wa pili wataondolewa ndani ya chama.

Alisema CHADEMA siyo chama cha kuendelea kuwa wapinzani. ‘’Tunajenga chama kinachokiandaa kushika dola muda wowote itakapopatikana fursa. Tunataka kuithibitishia dunia kwamba tunaweza kuongoza dola muda wowote zaidi ya CCM’’ Alisema Lowassa.