Huwezi Amini Kuwa Lowassa Sio Sababu ya Dk. Willibroad Slaa Kutoonekana Hadharani na Kwenye Vikao vya Chama..Sababu Hii Hapa - MULO ENTERTAINER

Latest

4 Aug 2015

Huwezi Amini Kuwa Lowassa Sio Sababu ya Dk. Willibroad Slaa Kutoonekana Hadharani na Kwenye Vikao vya Chama..Sababu Hii Hapa

Wakati maelfu ya watu nchini wakiamini kutoonekana hadharani kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibroad Slaa kunatokana na kuchukizwa na kitendo cha kukaribishwa kwa waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa , ukweli wa jambo hilo umeibuliwa.

Mjumbe mmoja wa Kamati Kuu (CCM) ya chama hicho amesema, madai yanayotolewa na watu mitaani na katika mitandao ya kijamii yakisema Dk. Slaa amekasirishwa na kitendo hicho ni ya uongo.

“Kwa taarifa yako, Dk. Slaa ndiye aliyemtaka Lowassa ajiunge Chadema. Mbowe (Freeman, Mwenyekiti wa Taifa Chadema) hakumtaka kabisa huyu jamaa aje kwetu. Kwa sababu hakuona jinsi gani wangewaeleza wananchi juu yake, lakini mzee ndiye aliyeshawishi na vikao vya kumjadili vikaanza mfululizo. Ukiangalia picha za awali, Dk. Slaa yupo.

Kinachotokea kwa Dk. Slaa ni shinikizo kutoka familia yake. Kuna watu walikuwa na matumaini makubwa ya kufaidika endapo yeye angegombea tena na kushinda urais mwaka huu, hivyo wameamua kununa kwa sababu kilichotokea hakina masilahi kwa familia." alisema mjumbe huyo wa kamati kuu