Nape Anasema Lowassa Amejivua Nguo...Najiuliza Alitegemea Aendelee Kuvaa Nguo Chafu? - MULO ENTERTAINER

Latest

4 Aug 2015

Nape Anasema Lowassa Amejivua Nguo...Najiuliza Alitegemea Aendelee Kuvaa Nguo Chafu?

Nape anasema Lowassa amejivua nguo...najiuliza alitegemea aendelee kuvaa nguo chafu? vazi la kijani alionyeshi uchafu na ndiyo maana upendelewa na Mafisadi. Ilikuwa ni jambo muhimu kwa Lowassa kuueleza umma juu ya Richmond na sasa tumejua. CCM na menejiment yake inawajibika kutoa maelezo ni wapi fedha za umma zilipelekwa. Tunamshukuru Mh. Lowassa kwani aliwajibika kwa mujibu wa sheria kuinusuru serikali na sasa ni wazi kabisa ni mtu safi haswa anapoendelea kuchukua maamuzi magumu ya kujiunga vema upinzani kuyakataa makabaila ndani ya CCM.