Hii Imekaaje Kwa Kijana Wetu Diamond platnumz...Atua Ujerumani na Timu Kubwa Kutoka Tanzania.. - MULO ENTERTAINER

Latest

18 Mar 2016

Hii Imekaaje Kwa Kijana Wetu Diamond platnumz...Atua Ujerumani na Timu Kubwa Kutoka Tanzania..

Katika kile kinacho itwa From Tandale to world tour,Diamond leo ametua Ujerumani kwaajili ya kukinukishaaa!

Lakini kilicho nishangaza ni kundi kubwa la watu alio nao,Sina kinyongo nao sababu wote nilio waona wanaumuhimu wake kwa huko aliko enda lakini najiuliza malipo ya show yake Moja yatakuwa yanamlipa sana hadi anweza kufanya hivi

Nimeona yupo na Mama ake its gud kwa shida walizo pitia na mama ake sasa niwakati wao wakula mema ya dunia amefanya kitu kizuri sana,Mwingine nimemuona Mke wake na mwanae nayo haina tatizo ni kizuri kwa mapenzi alio nayo kwa mke wake na mwanae,Nimemuona Rommy Jons naye hana shida ndo official Dj apart from kuwa na undugu na Diamond,

Nimeona Babu tale na Sallaam wote ni Mamanager wake its gud nayo,Nimewaona Madancer wake wanne yaah nao ni muhimu ukizingatia kuwa wanapiga sana kazi,nimeona Maphotographer wake akiwemo Kifesi ya nimuhimu kwa picha na Video kwa mashabiki

Sasa swali langu ni kuwa hivi hizi show Diamond zinamlipa sana hadi kufikia kuwa na watu wengi hivyo ambao anawagharamia kuanzia ticket za ndege Go and return ambapo kwenda nauli inaweza kuwa zaidi ya 2M kwa kichwa kimoja,atawagharamia malazi na chakula,Kuna wanao tegemea kulipwa hapo kama madancer,Dj,na Maphotographer,bado kuna zile bata ndogo ndogo na watakaa si chini ya Siku mbili!

Inaonekana Diamond hizi show Zina mlipa sana kwa hili la leo alilo tuonesha ni salamu tosha kwa Wasanii wengine kuwa Mziki unalipa na waache kulemba kwenye Game,kumbuka apo atagharamia mavazi ya kwenye show daaaa Diamond tunyooosheee

Zaidi ya watu kumi kweli Diamond kiboko Tunyooshe