UONGOZI wa Azam FC umeweka bayana kuwa, kocha wa timu ya Singida United, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, ndiye aliyeandika barua ya maombi ya kuifundisha timu yao tangu akiwa Yanga.
Pluijm ambaye ameanza kuinoa Singida United msimu huu, taarifa za uhakika zinasema kuwa Mholanzi huyo ameshasaini mkataba wa miaka miwili na matajiri hao wa Chamazi.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Meneja wa Azam FC, Philipo Alando, alisema kuwa kocha huyo ndiye aliyeandika barua kuwa anataka kuifundisha klabu hiyo tangu kipindi anaifundisha Yanga.
“Pluijm yeye ndiye aliyeandika barua kuwa anatamani kuja kutufundisha na mara ya kwanza aliandika akiwa anaifundisha timu ya Yanga kwa vile amemaliza mkataba na Singida ndiyo maana watu wanamhusisha kuja kwetu ila sisi huwa hatufichi kitu kama mlivyoona kwa Ngoma (Donald), sisi huwa tunaweka vitu hadharani,” alisema Alando.
29 May 2018
New
Azam FC yafunguka Pluijm aliomba kuifundisha timu yetu
mulo
Newer Article
Watoto Sita Wafariki Katika Ajali ya Gari Tanga
Older Article
Wachezaji 10 Yanga SC hawana mikataba
Atletico Madrid 'Yamfukuza' Diego CostaApr 27, 2019
Uganda Watuma Salamu kwa Taifa StarsMar 23, 2019
Labels:
AZAM SPORTS,
Michezo