Ukistaajabu ya Mussa Utayaaona ya filauni Aunt Ezekiel akana kuwa ana ujauzito baada ya kuhojiwa na Soud Brown ktk XXL ya Clouds Fm - MULO ENTERTAINER

Latest

16 Jan 2015

Ukistaajabu ya Mussa Utayaaona ya filauni Aunt Ezekiel akana kuwa ana ujauzito baada ya kuhojiwa na Soud Brown ktk XXL ya Clouds Fm


Jumatano ya January 14, kwenye XXL ya Clouds FM Soudy Brown amepiga story na muigizaji Aunty Ezekiel kuhusiana taarifa kwamba ni mjamzito na ameonekana akinywa pombe,

Soudy alimuuliza kama anafahamu athari za kunywa pombe huku akiwa na ujauzito, Aunty akasema hazijui na yeye sio mjamzito.

Soudy alimtafuta pia Dk Makongoro  kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili ambaye alielezea kuhusu matatizo ambayo mwanamke anaweza kuyapata iwapo ni mjamzito na anatumia pombe kali,

Daktari huyo amesema kuwa mama mjamzito anatengeneza mazingiza ya pombe kusafiri kutoka kwake kwenda kwa mtoto na kujitunza kwenye sehemu za ubongo kitendo kinachosababisha mtoto kuzaliwa akiwa na matatizo  kama mtindio wa Ubongo, Kuzubaa au matatizo ya macho.

----------------------
'You've gotta dance like there's nobody watching,
Love like you'll never be hurt,
Sing like there's nobody listening,
And live like it's heaven on earth.'