VIDEO: Television Kenya Zanasa Jinsi Simba Aliyetoroka Mbugani Nairobi Alivyouwawa Kwa Risasi Uraiani - MULO ENTERTAINER

Latest

31 Mar 2016

VIDEO: Television Kenya Zanasa Jinsi Simba Aliyetoroka Mbugani Nairobi Alivyouwawa Kwa Risasi Uraiani

Mwaka huu nimeziona mara tatu taarifa za habari kuhusu Simba kutoroka kwenye hifadhi ya Wanyama Nairobi Kenya na kuingia Uraiani na kufanya maisha kuwa ya wasiwasi, wengine wawili walitoroka kwenye mbuga hiyo kipindi kilichopita na kukutwa wakizurura kwenye foleni ya magari.

Hii video hapa chini inaonyesha jinsi Simba huyu alivyouwawa March 30 2016 na ni baada ya kuingia mtaani na kujeruhi mtu ambaye inaripotiwa alikimbizwa Hospitali kupata matibabu ambapo wiki mbili zilizopita Simba mwingine alijeruhi mtu kabla ya kukamatwa na kurudishwa kwenye hifadhi.